Pages

MUHAMBA

MUHAMBA
MUHAMBA HERBAL PRODUCTS

A.J.T.C

A.J.T.C
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE

Wednesday, 12 November 2014

KIFO CHA PILI CHARIPOTIWA MALI KUTOKANA NA UGONJWA WA EBOLA

NA ESTHER A CHAVALA.
 
12 Novemba 2014


 tarangiremedia.blogsports.com

Muuguzi kutoka nchini Mali amekufa kutokana na ugonjwa wa Ebola, kikiwa ni kifo cha pili tangu  Ugonjwa huo kudhibitishwa nchini humo.


Maafisa wanasema kuwa muuguzi huyo alikuwa amemtibu raia aliyewasili nchini humo kutoka Guinea katika kituo cha afya cha Pasteur jijini Bamako, kituo ambacho kwa sasa kimewekwa karantini.

Kesi hii haihusiani na ya kwanza ambayo msichana mwenye umri wa miaka miwili alikufa kutokana na Ebola mwezi oKtoba.

Shirika la Afya Duniani limetangaza mlipuko huu wa Ebola kama wa dharura duniani ambapo
Mtoto wa miaka miwili ndiye alikuwa wa kwanza kufariki kutokana na Ebola nchini Mali
tarangiremedia.blogsports.com

                              Mtoto wa miaka miwili aliyefariki mwezi octoba.
 
Kesi hii ya Mali imeibuka siku moja baada ya shirika la Afya Duniani kuwatoa watu ishirini na tano karantini waliodhaniwa kumkribia msichana wa miaka miwili aliyefariki oktoba .

Miongoni mwa watu 100 waliokuwa karantini wameelezea kuwa kisa cha mtoto huyo kuugua na kufariki kutokana na Ebola kimewashangaza sana maafisa wakuu kwani inaarifiwa alisafiri kwa basi kutoka mjini Bamako kuelekea Guinea.

Takriban watu 5,000 wamefariki Afrika Magharibi kutokana na ugonjwa  huo wa  Ebola.

CHANZO CHA HABARI BBC SWAHILI.

0 comments:

Post a Comment

AJTC

AJTC
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLEGE