Pages

MUHAMBA

MUHAMBA
MUHAMBA HERBAL PRODUCTS

A.J.T.C

A.J.T.C
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE

Wednesday, 12 November 2014

FIKRA ZA OSAMA ZAFUNZWA KWA WATOTO PAKISTANI


NA EMMA MOSHI


  • 12 Novemba 2014

 tarangiremedia.blogsports.com


Kiongozi wa kidini nchini Pakistani Abdul Aziz Ghazi anayemiliki shule nane zinazofundisha msimamo wa Bin Laden anatoa mafunzo ya fikra za Osama bin Laden kwenye shule za dini kwa Wanafu
nzi takriban 5,000.

Ingawa serikali ya nchi hiyo inapambana na wanamgambo wa Taliban kaskazini magharibi mwa Pakistani, haina mipango ya kuzifungia shule hizo zinazotoa elimu kwa watoto kuunga mkono wanamgambo wa Taliban.

Imamu wa msikiti mmoja mjini Islamabad Abdul Aziz Ghazi amesema wana malengo sawa na Taliban lakini amesema hawatoi mafunzo ya kijeshi.

Kiongozi huyo amesema wanatoa mafunzo kuhusu misingi ya Jihad ila ni juu ya wanafunzi kupata mafunzo ya kijeshi baada ya kutoka shuleni hapo.

Ghazi ambaye  anamiliki shule nane za kidini yaani Madrasa,moja ya shule yake iliwahi kufanya ziara ya kwenda kukutana na Osama Bin Laden nchini Afghanistan.

Hivi sasa wasichana 3,000 na wavulana 2,000 wanasoma kwenye taasisi zake ambapo mitaala ya shule zake inatoa mafunzo ya kusoma Quran, kiarabu na thiolojia,hesabu na sanaa inaonekana kuwa masomo ya kidunia, vitabu vingi vimeandikwa na Ghazi na kuchapishwa katika shule hizo zenye vyumba vya kuchapisha.

Hata hivyo  moja ya shule, zinazomilikiwa na Ghazi kuna maktaba iliyopewa heshima ya jina la bin Laden kutokana na ziara ya kwenda kumtembelea kiongozi huyonchini Afghanistan.

CHANZO CHA HABARI BBC SWAHILI
.

0 comments:

Post a Comment

AJTC

AJTC
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLEGE