Pages

MUHAMBA

MUHAMBA
MUHAMBA HERBAL PRODUCTS

A.J.T.C

A.J.T.C
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE

Wednesday, 12 November 2014

UNHCR kumaliza tatizo la wasio na Uraia

Mkutano wa UNHCR ulioanzisha kampeni dhidi ya hali ya kutokuwa na uraia

NA; SINYATI KILUSU
Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Wakimbizi-UNHCR limeanzisha kampeni inayolenga kumaliza tatizo la watu wasio na uraia, ambao kwa mujibu wa shirika hilo wanafikia milioni 10 kote ulimwenguni.
Mkutano wa UNHCR ulioanzisha kampeni dhidi ya hali ya kutokuwa na uraia
Kampeni hiyo imeanzishwa chini ya kaulimbiu ijulikanayo kwa lugha ya kiingereza kama ''I belong''. Shirika la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Wakimbizi-UNHCR limesema kupitia kampeni hiyo linataka kuzimulika changamoto wanazokabiliana nazo watu wasio na uraia, na kuzihimiza nchi kuzirekebisha sheria zao ili asiwepo mtu anayejikuta katika hali ya kutokuwa raia wa nchi yoyote.
Mkurugenzi wa UNHCR Antonia Guterres amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, kwamba kila dakika 10 anazaliwa mtu asiyekuwa na uraia wa taifa lolote ulimwenguni, na kwamba kutokuwa na uraia huwafanya watu hao kuhisi kama kuwepo kwao ni makosa. Guterres ameongeza kuwa hilo halikubaliki katika karne ya 21.
''Watu wasio na uraia hunyimwa haki zao za kimsingi, kama vile kuandikishwa kisheria wanapozaliwa, kwenda shule, huduma za afya, ndoa na nafasi za ajira, na hata kunyimwa hati ya kifo pale wanapoiaga dunia'', imesema ripoti ya shirika hilo.
Ukosefu wa uraia hutokana na sababu nyingi
Watu wa jamii ya Rohingya: Myanmar na Bangladesh zimekuwa zikiwatupiana kama mpira
Watu wa jamii ya Rohingya: Myanmar na Bangladesh zimekuwa zikiwatupiana kama mpira
Watu wanaweza kunyimwa uraia kutokana na sababu mbali mbali, zikiwemo za ubaguzi wa kikabila, wa kimadhehebu na hata wa kijinsia. Hali hiyo
pia
yaweza kutokea pale mataifa yanaposambaratishwa na vita au mizozo.

Idadi kubwa ya watu wasio na uraia hupatikana nchini Myanmar, ambako serikali ya nchi hiyo haiwatambui watu wa jamii ya Rohingya ambao ni waislamu. Guterres amesema idadi ya watu hao ni takribani milioni moja.
Myanmar huwachukulia watu hao kuwa wahamiaji kutoka Bangladesh, nchi ambayo pia huwachukulia wale wanaovuka mpaka kutoka Myanmar kuwa wahamiaji haramu.
Kusambaratika kwa mataifa
Idadi nyingine kubwa ya watu wasio na uria wapatao 600,000 ilitokana na kuvunjika kwa Muungano wa Kisovieti wa Urusi miaka zaidi ya 20 iliyopita.
Changamoto za kukosa uria pia huwakumba watu waliozikimbia nchi zao. Kwa mfano, asilimia 70 ya watoto wanaozaliwa na wakimbizi kutoka Syria walioko Lebanon na Jordan hawapati vyeti vya kuzaliwa, amesema Antonio Guterres

chanzo DW SWAHILI

0 comments:

Post a Comment

AJTC

AJTC
ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLEGE